Alhamisi, 21 Novemba 2013

VIJUE VIWANJA KUMI BORA NA VYENYA MWONEKANO MZURI ZAIDI DUNIANI

Namba 10

 Estadio Azteca, Mexico City, Mexico

Kiwanja hiki ndicho kilichochezewa fainal ya kombe la dunia mwaka 1970 na mwaka 1986 wakati Nchi ya mexico ilipo andaa michuano hiyoo mikubwa kabisa duniani. kati ya ITALIA na BRAZIL mchezo uliomalizika kwa brazili kunyakua kombe hilo baada ya ushindi wa goli 4 - 1.

 

Kiwanja hiki cha Azteca kina uwezo wa kubeba watazamaji wasiopungua laki moja (100,000) walioketi kwenye viti. 

 

 Kiwanja hiki kina nyasi marizawa za kupandwa katika eneo lake la kuchezea (pitch)

 

 

Namba 9

 Nou Camp, Barcelona, Spain

Kiwanja hiki kinachomilikiwa na klabu ya brcelona ya Uhispania ambacho kilichezewa fainali ya klabu bingwa ya ulaya mwaka 1999 kati ya MANCHESTER UNITED na BUYERN MUNICH na manchester kutwaa ubingwa huo kwa ushindi wa goli 2 - 1. Ujenzi wa uwanja huu ulimalizika mnamo mwaka 1957 na uligharimu kiasi cha dola za kimarekani milion 3, Hadi sasa uwanja huu ndio mkubwa kuliko yote barani ulaya.

 

Kiwanja hiki kinachukua watazamaji laki moja na ishirini elfu (120,000) walioketi kwenye viti hadi kufikia tafiti zilizofanywa na UEFA hivi karibuni

 

 

Kiwanja hiki kina nyasi maridhawa za kupandwa katika eneo lake la kuchezea (pitch) zinazowawezesha wanandinga kupiga pasi watakavyoo.

Namba 8

 Old Trafford, Manchester, England

Kiwanja hiki kina milikiwa na mabingwa mara 20 wa ligi kuu ya Uingereza na mabingwa mara 2 UEFA champions league. kiwanja hiki kilikamilisha ujenzi wake na kuanza kutumiwa na man mnamo mwaka 1910.   

 

Kiwanja hiki kin uwezo wa kubeba watazamaji walioketi kwenye viti takribani elfu sabini na nane (78,000) tofauti na miaka ya nyuma wakati ulikuwa unabeba watu elfu sitini na nane (68,000).

Kiwanja hiki kina nyasi maridhawa za kupandwa katika eneo lake la kuchezea (pitch) ambazo hung'olewa na kupandwa upya kila baada ya msimu kumalizika

Namba 7

Estadio Santiago Bernabeu, Madrid, Spain

Kiwanja hiki kina milikiwa na klabu ya Real Madrid ya Uhispania. Ni kiwanja chenye historia lukuki na za kuvutia ambacho kilipewa jina na mwasisi wake Bw. Santiago Bernabeu mwaka 1953 baada ya kuhama kwenye kiwanja chao cha awali  Chamartin Stadium kilichoharibiwa na vita ya wenyewe kwa wenyewe mwaka 1924.

 

 

kiwanja hiki niuwezo wa kubeba watazamaji wasio pungua elfu themanini na tano mia nne hamsini na nne(85, 454) walio keti kwenye viti.


 

Kiwanja hiki kina nyasi maridhawa za kupandwa katika eneo lake la kuchezea (pitch)ambazo hufanyiwa matunzo na jopo la wataalamu kutoka kitivo cha nyasi katika chuo kikuu cha hispania.

Namba 6

Louis II, Monte Carlo, Monaco

uwanja huu unamilikiwa na klabu ya AS Monaco ya Ufaransa upo pembezoni  ya jiji la monaco nchini ufaransa ni moja kati ya viwanja vivutio duniani kwani kipo karbu na ukwe  maarufu nchini ufarasa. kilijengwa mnamo mwaka 1937.

 

 

Kiwanja hiki kina uwezo wa kubeba mashabiki takribani elfu ishirini (20,000) walioketi kwenye viti. Pamoja na udogo wa uwanja huu bado unabaki kuwa moja ya viwanja vinavyovutia zaidi duniani.

 

 

 

Kiwanja hiki kina nyasi maridhawa za kupandwa katika eneo lake la kuchezea (pitch) maalumu zilizoagizwa kutoka Falme za Kiarabu na Abu Dhabi

Namba 5

San Siro, Milan, Italy

Kiwanja hiki kina milikiwa na klabu mbili hasimu zaidi nchini Italia AC Milan na Inter Milan. Katika uwanja huu kila kitu ni kandanda, kabumbu, mpira au soka ni moja kati ya vuwanja vyenye historia kubwa duniani. Mashabiki wendawazimu wa soka wanapatikana kaika dimba hilo.

 

Kiwanja hichi kilijengwa na uwezo wa kubeba mashabiki elfu themanini (80,000) walio kaa kwenye viti hivyo hauna barabara za kukimbilia kuuzunguka uwanja
Kiwanja hiki kina nyasi maridhawa za kupandwa katika eneo lake la kuchezea (pitch) 

 

Namba 4

Maracana, Rio De Janeiro, Brazil

Kiwanja hiki kinamlikiwa na timu ya taifa ya Brazili ni moja kati ya viwanja bora na vyenye mvuto wa kipekee duniani. Ndio uwanja uliowahi kuingiza watazamaji wengi zaidi duniani takribani 200,000 kwenye fainali za kombe la dunia mwaka 1950, Huku brazili akiwa mwenyeji. Kiwanja hiki kilijengwa maalumu kwaajili ya michuano ya mwaka 1950 na kiligharimu dola za kimarekani milioni 40.
Kiwanja hichi kina uwezo wa kubeba watazamaji laki moja ishirini na tano elfu (125,000) waliokaa kwenye viti na watazamaji zaidi ya elfu thelathin na moja mia saba arobaini (31,740) waliosimama.
Kiwanja hiki ina nyasi asilia za kupandwa zilizokatwa kwa mtindo wa drafti katika sehemu ya kuchezea (pitch).

 
    

Namba 3

Stadio Olimpico, Rome, Italy

Kiwanja hiki kinachomolikiwa na AS Roma awali kilijengwa kwaajili ya mashindano ya olimpiki mwaka 1960 ila baada ya hapo kilionekana kinafaa kwaajili ya michezo ya soka hasa baada ya kujengewa paa la juu na mara kadhaa umetumika kwenye mechi za timu ya taifa ya Italia.
Kiwanja hichi kina uwezo wa kubeba watazamaji Elfu themanini na mbili na mia tatu (82,300) waliokaa kwenye vit.

 

Kiwanja hiki kina nyasi asilia za kupandwa katika eneo la kuchezea (pitch) ambazo zimekatwa kwa mtindo wa kuzunguka sehemu ya katikati ya kiwanja.

 

Namba 2

Azadi, Tehran, Iran

Linaweza kwa jambo la kushangaza katika medani ya soka juu ya nchi kama Irani kumiliki moja kati ya viwanja bora kabisa vya soka duniani lakini ndo hali halisi kiwanja hiki cha Azadi kijitengenezwa mwaka 1974 kwaajili ya michuano ya bara la Asia .

 

 

kiwanja hiki kina uwezo wa kubeba watazamaji wasiopungua laki moja na ishirin (100,020) walioketi kwenye viti na zaidi ya idadi ya elfu thelathini (30,000) waliosimama

 

Kiwanja hiki kina nyasi asilia za kupandwa katika eneo lake la kuchezea (pitch) ambazo zimekatwa kwa mtindo wa mistari sambamba ambayo unauongezea unadhafu uwanja huo.

 

 

Namba 1

International Stadium Yokohama, Yokohama, Japan

Kiwanja hiki ndicho kilichochezewa fainali ya kombe la dunia mwaka 2002 kati ya Ujerumani na Brazili. kiwanja hiki hadi kukamilika kwake kiligarimu Yen bilioni 60 na ndicho kiwanja kikubwa zaidi nchii Japani.

Kiwanja hiki kinauwezo wa kubeba watazamaji walioketi kwenye viti elfu sabini (70,000)

Kiwanja hiki kina nyasi asilia za kupandwa katika eneo la kucheea (pitch) ambazo haziwezi kukauka katika kipindi cha kiangazi maana nchini ardhini zimetandazwa bomba maalumu kwaajili ya kutoa mvuke utakaoendeleza ukuaji wa kiwanja hicho.

Je unadhani list hii ipo sahihi toa maoni yako na wewe na list yako nasi tutaitolea ufafanuzi na kuibandika kwenye blog yetu hii.


Hakuna maoni:

Chapisha Maoni